Bwana atuita Bwana Yesu atuita, tujongee mbele yake, tukampokee x2
Mwili wako, ee Bwana, damu yako, ee Bwana, vyatushibisha roho zetu x2
Karamu yako ni chakula cha kweli, karamu yako ni kinywaji cha kweli.
Karamu yako ni kumbukumbu la mateso yako, karamu yako ni karamu ya sadaka.
Karamu yako ni Mwanakondoo kweli wa Pasaka, karamu yako ni mana kweli katika safari yetu
Karamau yako ni amana ya ufufuko wetu, karamu yako ni mfano wa karamu ya mbinguni
Karamu yako ni dawa ya udhaifu wetu, karamu yako ni malisho ya mchungaji mwema.
コメント