top of page

Bubujiko

Damu imebubujika, Ni ya Imanweli,

Wakioga wenye taka, Husafiwa kweli.


Ilimpa kushukuru Mwivi mautini;

Nami nisiye udhuru, Yanisafi ndani.


Kondo-o wa kuuawa, Damu ina nguvu,

Wako wote kuokoa Kwa utimilivu.


Bwana, tangu damu yako Kunisafi kale,

Nimeimba sifa zako, `taimba milele.


Bwana, umenikirimu Nisiyestahili

Kwa damu yako, sehemu Ya mali ya kweli.


Nikubali kukwimbia Mbinguni milele.

Mungu nitamsifia Jina lako pweke.

0 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page