Damu imebubujika, Ni ya Imanweli,
Wakioga wenye taka, Husafiwa kweli.
Ilimpa kushukuru Mwivi mautini;
Nami nisiye udhuru, Yanisafi ndani.
Kondo-o wa kuuawa, Damu ina nguvu,
Wako wote kuokoa Kwa utimilivu.
Bwana, tangu damu yako Kunisafi kale,
Nimeimba sifa zako, `taimba milele.
Bwana, umenikirimu Nisiyestahili
Kwa damu yako, sehemu Ya mali ya kweli.
Nikubali kukwimbia Mbinguni milele.
Mungu nitamsifia Jina lako pweke.
Comments