top of page

Ati tuonane

Ati tuonane mtoni? Maji mazuri ya mbingu;

Yanatokea mwangani, penye kiti cha Mungu.


Naam, tuonane mtoni! Watakatifu, kwenu ni mtoni!

Tutakutanika kule mtoni penye kiti cha Mungu.


Tukitembea mtoni na Yesu Mchunga wetu,

Daima tu ibadani usoni pake kwetu.


Tukisafiri mtoni tutue ulemeao

Wema wa Mungu yakini; una taji na yao!


Kwang`ara sana mtoni cha Mwokozi ni kioo,

Milele hatuachani tumsifu kwa nyimbo.


[5]

Karibu sana mtoni, karibu tutawasili,

Mara huwa furahani na amani ya kweli.

8 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page