Enyi viumbe vyote- Twendeni mbele zake Bwana
Kwa moyo wa shukrani-Twendeni mbele zake Bwana
Twakushukuru- Ee Yesu twakushukuru sana x2
Kwa zawadi ya maisha na Baraka wanikirimia, ni upendo wa ajabu ulonipa Ee Mungu wangu
Nitaimba kushukuru kwa sauti na ala tamu jina lako litukuzwe milele na hata milele asante Yesu wangu asante Yesu wangu x2
Twakushukuru Ee Yesu twakushukuru sana
1. Kwa kinywa changu nitakushukuru na kukuimbia, kwa wema wako ulonijalia maishani mwangu…
Asante Ee Yesuasante sana Ee Yesu Asante sana.
2. Uliyonipa ni mengi sana siwezi kuhesabu, kwa wema wako ulinijalia mimi mja wako…
Asante Ee Yesuasante sana Ee Yesu Asante sana.
3. Nakurudishia sifa na utukufu ewe Mungu ae uhimidiwe milele yote uhimidiwe Bwana…
Asante Ee Yesuasante sana Ee Yesu Asante sana.
Comments