top of page

Anakuja Bwana Yesu

Pengine ni saa ya kupambazuka,

Mishale ya jua ipenyapo giza,

Kwamba atakuja Yesu mtukufu,

Awapokee wake.


Bwana itakuwa lini Tutapoimba,

‘Anakuja, Bwana Yesu, Aleluya,

Amin, Aleluya, Amin?‘


Pengine mchana, pengine jioni,

Pengine usiku wa manane, giza,

Itatoweka kwa fahari akija,

Awapokee wake.


Majeshi yake yataimba ‘Hosana,‘

Na watakatifu waliotukuzwa,

Watamsifu kwa kuwa amekuja,

Awapokee wake.


Furaha tukiitwa pasipo kufa,

Pasipo kuona maradhi, machozi;

Kuchukuliwa winguni kwa fahari,

Akija kwa watu wake.

3 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page