Amezaliwa Masiha wetu, hoyee hoye hoye Mwana wa Mungu mkombozi wetu, hoyee hoye hoye Leo kazaliwa naye Maria na amelazwa kwenye hori la wanyama, twende tukamwone Amekuja kwetu mwana wa Mungu kuzichukua dhambi zetu wanadamu, mkombozi wetu { Tumsujudie Bwana Mungu, kwa vigelegele Tucheze ngoma na kayamba tupige makofi } *2
Amelala manyasini, twendeni tukamwone, tukamsalimie Mkombozi wetu kwa zawadi zetu za dhahabu uvumba na manemane
Wachungaji waondoka, waenda Bethlehemu, Wakamsujudie Bwana Mkombozi, wafurahi naye pamoja na Maria naye Yusufu
Malaika wamefika wengi na wa mbinguni tukajiunge nao tuimbe pamoja utukufu uwe kwa Mungu juu amani kwa watu wenye mapenzi mema
Tumpokee mkombozi Masiha amekuja ewe mtoto Yesu ishi ndani yetu, tuangaze sisi, kwa mwanga wako mwanga wa Mbinguni.
Comments