[s/a] Bwana Utuhurumie, (ee Bwana)
[w] Bwana utuhurumie x2
[t/b] Kristu utuhurumie, (ee Kristu)
[w] Kristu utuhurumie x2
Bwana ….
UTUKUFU
1. Utukufu kwa Mungu juu mbinguni Na amani kote duniani (Kwa watu) wenye mapenzi mema Tunakusifu Baba, tunakuheshimu, Twakuabudu sisi tunakutukuza 2. Twakushukuru Mungu kwa ‘tukufu Wako mkuu ewe Mungu mfalme (Ee Baba) wa Mbingu Baba yetu
3. Bwana wetu mwokozi Yesu Kristu Mwana wa pekee wake Mungu (Uliye) Mwanakondoo wa Mungu
4. Unayeziondoa dhambi zote Za dunia utuhurumie (Pokea) pokea ombi letu
5. Wewe unayeketi kuume Kwake Baba utuhurumie (Sikia) sikia ombi letu
6. Kwani pekee yako ndiwe Bwana Pekee yako mkuu na mkombozi (Pekee) pekee Yesu Kristu
7. Kwa umoja wa Roho mtakatifu Ndani yake Baba watukuzwa (Ee Yesu) milele na milele
NASADIKI
Nasadiki kwa Mungu mmoja - Mimi nasadiki
Ndiye Baba yetu Mwenyezi “
Muumba mbingu pia dunia. “
Nasadiki kwa Yesu Kristu. “
Ninasadiki x2, mimi nasadiki (nasadiki ninasadiki) mimi nasadiki x2
Mwana wa pekee wa Mungu – Mimi nasadiki
Aliyezaliwa kwa Baba– Mimi nasadiki
Akapata mwili kwa Roh– Mimi nasadiki
Kazaliwa naye Bikira– Mimi nasadiki
Kisha yeye kasulibiwa – Mimi nasadiki
Kwa mamlaka yake Pilato– Mimi nasadiki
Kwa ajili yetu Kateswa – Mimi nasadiki
Alikufa na akazikwa– Mimi nasadiki
Kafufuka katika wafu – Mimi nasadiki
Akapaa juu mbinguni – Mimi nasadiki
Ameketi kuume kwake – Mimi nasadiki
Mungu Baba yetu Mwenyezi– Mimi nasadiki
Ndipo atakapotokea – Mimi nasadiki
Kuwa hukumu wote – Mimi nasadiki
Kwake Roho Mtakatifu– Mimi nasadiki
Kwa kanisa la Katoliki– Mimi nasadiki
Ushirika wa watakatifu – Mimi nasadiki
Ondoleo la dhambi zetu– Mimi nasadiki
Nangojea ‘fufuko wa miili – Mimi nasadiki
Na uzima wa milele– Mimi nasadiki
MTAKATIFU
Tenor: Mtakatifu, mtakatifu Bwana All: Mungu wa majeshi Sop: Mtakatifu Bwana All: Mungu wa majeshi S/A Mbingu na dunia zimejaa, zimejaa All: Mbingu na dunia , zimejaa utukufu wako S/A Mbingu na dunia All: Zimeja utukufu wako.
Hosana juu x4 mbinguni.
Mbarikiwa ‘naye kuja, mabrikiwa ‘naye kuja, mbarikiwa. Mbarikiwa ‘naye kuja kwa jina, jina lake Bwana.
FUMBO LA IMANI
Yesu Kristu alikufa, Yesu Kristu kafufuka, Yesu Kristu atakuja, atakuja kwetu tena.
BABA YETU
Baba yetu Baba wa mbinguni, jina lako Baba litukuzwe, Ufalme wako Baba na ufike, utakalo Baba lifanyike
Duniani kama mbinguni Ee Baba – Utakalo lifanyike
Tupe leo riziki zetu ee Baba – Utakalo lifanyike
Riziki zetu za kila siku Ee Baba – Utakalo lifanyike
Dhambi zetu utusamehe Ee Baba – Utakalo lifanyike
Kama vile twasamehe Ee Baba – Utakalo lifanyike
Waliotukosea sisi Ee Baba – Utakalo lifanyike
‘Situtie kishawishini Ee Baba – Utakalo lifanyike
Walakini utuopoe Ee Baba – Utakalo lifanyike
Maovuni utuopoe Ee Baba – Utakalo lifanyike
Kwa kuwa ufalme ni wako Ee Baba – Utakalo lifanyike
Nayo nguvu, na utukufu Ee Baba – Utakalo lifanyike
Daima daima milele Ee Baba – Utakalo lifanyike
AMINA
S/A Amina, Amina, All: Amina, Amina, Amina, Amina, x2
MWANA KONDOO
Tenor: Mwana Kondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia, All: Ee Mwana utuhurumie Sop: Mwana Kondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia All: Ee Mwana utuhurumie. Bass Mwana Kondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia All: Ee Mwana, utujalie amani
Comments