BWANA TUHURUMIE
Ee Bwana tuhurumie, ee Bwana ee,
Bwana tuhurumie
Kristu tuhurumie
Ee Kristu tuhurumie x3
UTUKUFU
Utukufu juu kwa Mungu mbinguni
Na amani duniani kwa watu wa mapenzi
wenye mapenzi mema. Tunakusifu (Baba) tunakuheshimu.
Tunakuabudu (Baba) tunakutukuza.
Baba tunakushukuru kwa ajili ya utukufu,
utukufu wako mkuu.
Ewe Mungu ni mfalme wa Mbinguni,
Mungu Baba, Baba ndiwe Mwenyezi.
Ewe Bwana Yesu Kristu ndiwe mwana
wake Mungu, ndiwe mwana wake Baba.
Ewe Bwana Mungu Mwana kondoo wake
Mungu, Mwana wake Baba
Ewe mwenye kuondoa zetu dhambi za
dunia, Bwana utuhurumie.
Ewe mwenye kuketi kuume kwake Baba,
ewe utuhurumie.
Ni kwa kuwa ndiwe uliye pekee yako
Mtakatifu, Bwana Yesu Kristu.
Na pamoja naye Roho Mtakatifu katika
utukufu wa Mungu Baba.
NASADIKI
Nasadiki kwa Mungu mmoja.
Nasadiki kwa Mungu mmoja
Muumba mbingu na dunia na kwa Yesu Kristu
mwanaye wa pekee Bwana wetu,
Nasadiki ninasadiki (mimi) kweli ninasadiki,
nasadiki kwa Mungu mmoja.
Alipata mwili kwa tendo lake Roho Mtakatifu, kazaliwa naye Bikira, akateswa kwa ponsio pilato.
Akasulibiwa akafa, akazikwa kaburini, na kuzimu akashukia,
kafufuka siku ya tatu.
Akapaa juu mbinguni, ameketi kuume kwa Baba, Mungu Baba yetu mwenyezi Muumba mbingu na dunia.
Ndipo atakapotokea kuhukumu wazima na wafu, na ufalme wake milele utakuwa bila mwisho.
Nasadiki kanisa ni moja, ni kanisa takatifu,
ni kanisa la katoliki ni kanisa la mitume.
Ushirika wa watakatifu, ondoleo la dhambi zetu, nasadiki ufufuko wa miili, na uzima wa milele.
HALLELUYA
Halleluyaia
Halleluia, alleluia (halleluia)
Halleluia halleluia x2
AMINA
Amina
Amina, amina (amina)
Amina, amina x2
MTAKATIFU
Mtakatifu Bwana
Mtakatifu Bwana, Mtakatifu Bwana
(Bwana) Mungu wa majeshi x2
Mbinguni na dunia zimejaa utukufu wako
hosanna juu mbinguni,
hosanna (hosanna) juu mbinguni.
Mbarikiwa ajaye kwa jina lake Bwana
Hosanna juu mbinguni,
hosanna (hosanna) hosanna juu mbinguni x2
BABA YETU
Baba yetu
Uliye juu mbinguni jina lako litukuzwe,
(Ee Baba)
Ufalmeo ufike utakalo lifanyike duniani
kama Mbinguni. Baba wa mbinguni jina
lako litukuzwe.
Utupe leo mkate, mkate wetu na utupe
tupe mkate wa kila siku. Baba wa
mbinguni jina lako litukuzwe.
Makosa tusamehe kama vile twasamehe
watu waliotukosea. Baba wa mbinguni
jina lako litukuzwe.
Usitutie penye kishawishi walakini
maovuni utuopoe. Baba wa mbinguni
jina lako litukuzwe.
Kwa kuwa ufal me ni wako na nguvu na
utukufu hata milele. Baba wa mbinguni
jina lako litukuzwe.
MWANAKONDOO
Mwanakondoo Mwana wa Mungu uondoaye dhambi za
dunia utuhurumie x2
Mwanakondoo, Mwana wa Mungu uondoaye dhambi za
dunia. Utuhurumie. Utujalie, utujalie, amani Utujalie, utujalie, utujalie amani. X3
Comments