top of page

Acheni Visingizio


Acheni visingizio wanadamu, acheni visingizio kwamba hali ni ngumu x2 Nendeni mkatoe (sadaka) nendeni mkatoe (sadaka), nendeni mkatoe sadaka kwa Bwana x2

  1. Siyo ninyi wenye magari ya kifahari mnaodai hali ni ngumu. Siyo ninyi wenye fedha nyingi mifukoni mnaodai hali ni ngumu.

  2. Siyo ninyi wenye majumba ya kifahari mnaodai hali ni ngumu. Ndani yake mmejaza vito vya thamani mnaodai hali ni ngumu.

  3. Siyo ninyi mnaovuna mazao mengi mnaodai hali ni ngumu. Siyo ninyi mnaopokea mishahara mnaodai hali ni ngumu.

  4. Msidhani mmepata kwa uwezo wenu mnaodai hali ni ngumu. Bali ni Mungu aliye wajalia hayo mnaodai hali ni ngumu.

  5. Kumbukeni mjane alotoa dinari mnaodai hali ni ngumu. Hakubakiza chochote mfukoni mwake mnaodai hali ni ngumu.

5 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page