Tumshukuru Mungu Baba yetu kwa zawadi zake zote tulizopewa bure. Kwa uzuri na maajabu ya uumbaji wako, katika ardhi na anga na bahari, Tunakushukuru, Bwana
Kwa yote ambayo ni neema katika maisha ya wanaume na wanawake, ikifunua sura ya Kristo,Tunakushukuru, Bwana
Kwa chakula na kinywaji chetu cha kila siku, nyumba zetu na familia, na marafiki zetu,Tunakushukuru, Bwana
Kwa akili za kufikiria, na mioyo ya kupenda, na mikono ya kutumikia,Tunakushukuru, Bwana
Kwa afya na nguvu ya kufanya kazi, na burudani ya kupumzika na kucheza,Tunakushukuru, Bwana
Kwa walio jasiri na hodari, ambao ni wavumilivu katika mateso na waaminifu katika shida,Tunakushukuru, Bwana
Kwa watafutaji wote mashujaa wa ukweli, uhuru, na haki,Tunakushukuru, Bwana
Kwa ushirika wa watakatifu, wakati wote na mahali pote,Tunakushukuru, Bwana
Zaidi ya yote, tunakushukuru kwa rehema kubwa na ahadi tulizopewa katika Kristo Yesu Bwana wetu; kwake na sifa na utukufu, pamoja nawe, Baba, na Roho Mtakatifu, sasa na hata milele. Amina.
Kwa jina la Baba, na la mwana na la Roho Mtakatifu. Amina